Papa awateka maaskofu kusaidia ushoga, utoaji mimba, talaka, na madawa ya uzazi wa mpango
Page 1 of 1
Papa awateka maaskofu kusaidia ushoga, utoaji mimba, talaka, na madawa ya uzazi wa mpango
"Papa Francis amewataka viongozi wa juu wa kanisa hilo kuzingatia Zaidi suala la wapenzi wa jinsia moja chanya kuliko kuwa kinza na amefanikiwa kuwateka maaskofu wanaohudhuria mkutano huo wa sinodi." —(BBC 15 Oktoba 2014)
Inashangaza kuona kwamba watu wengi bado wametekwa katika kanisa hili la kishetani, wakati unapoona kiongozi huyu ambaye kulingana na madogima ya kanisa, ni kiongozi mkuu, anafanya wazi wazi mambo kama haya: kuunga mkono mashoga, utoaji wa mimba, vidonge vya uzazi wa mpango, talaka, n.k.. Hii siyo tu kwamba wanafanya dhambi, lakini ni kumkana Yesu wazi wazi. Na hii ndiyo sababu wanawakataza makuhani wao kuoa kwa fundisho lao la "useja" lililotabiriwa na Paulo kwamba siku zijazo mafundisho ya kishetani katika kanisa la mpingakristo yangewazuia watu kuoa (angalia 2Timotheo 1:2). Kwanini wanawakataza makuhani wao kuoa, wakati bado wanasaidia ndoa za jinsia moja? Ni wazi kwamba wao wenyewe ni mashoga na wasagaji, na wakati linapokuja swala la ndoa za jinsia moja, hawawezi kufanya chochote ila kuliunga mkono. Hii inathibitishwa kama ilivyo wazi makuhani wa katoliki wengi ni wasagaji na mashoga, na kanisa katoliki linaongoza kwa kesi nyingi za usagaji huko marekani.
Lakini kinachonishangaza ni kwamba, roho nyingi za waaminifu bado zimetekwa katika jumuiya hii, na wakati ukiwaambia Wakatoliki kwamba papa ni mpingakristo, watakuchukia kwamba unahukumu wakati unawambia ukweli. Matunda ambayo papa huyu na maaskofu wake wanazaa, yanatosha kuthibitisha kwamba ni matunda ya mpingakristo. Na kama Yesu alivyosema kwamba jumuiya ya mpingakristo tunaweza kuitambua kwa matunda yao tu. Na matunda yao yanawaweka wazi kwamba ni wapingakristo.
Kama ukisoma zaidi habari hiyo niliyotoa hapo juu katika kiungo hiki, utaona kwamba papa analalamika kwamba baadhi ya wakatoliki sasa wanaliacha kanisa kwa sababu ya mafundisho haya ya ushoga, na talaka, na utoaji mimba. Hii ni sahihi kwa mkatoliki yeyote mwaminifu; kwa maana huwezi kushiriki katika mambo ya giza kama hayo.
Waefeso 5:11 "Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;"
" />
Similar topics
» Ajenda ya papa ya mabadiliko ya tabia nchi itasababisha kupitishwa kwa sheria ya Jumapili.
» Papa Francis asema haoni tatizo kwa wachungaji na makasisi ambao ni mashoga.
» Papa Francis asema haoni tatizo kwa wachungaji na makasisi ambao ni mashoga.
Page 1 of 1
Permissions in this forum:
You cannot reply to topics in this forum
|
|